Jumapili, 15 Oktoba 2017

CHAPISHA KITABU KWA SHILINGI ELFU THEMANINI



Idadi  kubwa  ya  waandishi chipukizi  nchini  Tanzania, wanakabiliwa  na  changamoto  moja  kubwa. Nayo si nyingine  isipokuwa  ni kushindwa  kufikia  ndoto  ya  kuchapisha  walau  kitabu kimoja   kwa   sababu  ya  kutokumudu  gharama  za  uchapishaji  wa vitabu.

Kuchapisha  kitabu  chenye  kiwango  ( standard ) kinacho  hitajika  sokoni, ambacho  kinaweza  kukubaliwa  na  wauzaji  na  wasambazaji  wakubwa nchini,  mwandishi  anatakiwa  kwa  kadirio la  chini  kabisa,  awe  na  walau  kiasi  cha  shilingi  LAKI  NANE  hadi  MILIONI  MOJA NA NUSU kutegemea  na  ukubwa  wa  kitabu.

Kiasi  hiki  kinaonekana  kuwa  kikubwa  mno  kwa mwandishi  chipukizi  ambae  ndio  kwanza  anataka  kutumia  kipaji  chake  cha  uandishi kujipatia  fedha  kwa  ajili  ya  kuendesha maisha  yake ya  kila  siku   na  kupata maendeleo  kwa  ujumla.

Mwisho  wa  siku  waandishi  hawa  huamua  kukata  tamaa  ya  kutimiza  ndoto  yao  hiyo  adhimu  na  matokeo  yake  mawazo  waliyo  taka  kuyaandikia  kitabu hufa  ama kupotea.

SULUHISHO   LA   CHANGAMOTO   HII

Katika kukabiliana  na  changamoto  hii, kampuni  ya  masoko  ya  MWALU MARKETING  & GENERAL ENTERPRISES   imenzisha  program  maalumu  ya  kuwasaidia  waandishi chipukizi  kuchapisha  mawazo  yao  kwenye  kitabu  kwa  gharama  nafuu  kabisa  ambazo  wanaweza  kuzimudu.

Badala  ya  mwandishi  mmoja, kutoa  gharama  ya  SHILINGI  LAKI NANE  kwa  ajili  ya  kuchapisha  kitabu  chake,  Mwalu  Marketing  inawakusanya  waandishi  chipukizi  kuanzia  kumi  wenye  mawazo  yanayo  fanana  na  kuchapisha  kitabu  kimoja  ambapo  kila  mwandishi  atatakiwa  kutoa  kiasi  cha  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tshs . 80,000/=).

Program  hii imelenga  kuwasaidia  maelfu  ya  waandishi  chipukizi  wa   vitabu  nchini  Tanzania, ambao  wanatamani  kuyaweka mawazo  yao  kwenye  vitabu   lakini  wanashindwa  kwa  sababu  tu hawana uwezo  wa  kumudu  gharama kubwa  za  uchapishaji.

TUNAPOKEA  MAOMBI  YA  WAANDISHI  CHIPUKIZI  WANAO  TAKA KUSHIRIKI  KATIKA PROGRAMU.
Kama  wewe  ni  mwandishi chipukizi  ambae  unatamani  kuchapisha  kitabu  ama  kuweka  wazo  lako  kwenye  kitabu  lakini   hauna  pa kuanzia  kwa  sababu  ya  kutokuwa na  uwezo  wa  kumudu  gharama kubwa  za  uchapishaji, basi  hii  ni  HABARI NJEMA  SANA  KWAKO. 
Kwani kupitia  program  hii, utaweza  kuweka  wazo  lako  kwenye  kitabu  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  THEMANINI  TU (Tshs.80,000/=)

                                    SIFA   ZA  MAUDHUI  YA   KITABU

Ili kitabu  chako  kiweze  kukwekwa  kwenye  program  hii  ni lazima  kiwe  na  sifa zifuatazo :
1.    Kiwe  na  maudhui  mazuri  na yenye  kuvutia yasiyo  kinyume  na  maadili  ya  mtanzania.
2.    Kiwe  na maudhui  yanayo zingatia   na  kufuata  taratibu  na sheria za  nchi.
3.    Kisiwe  na  maudhui  ya kisiasa  au  yenye  mwelekeo  wa  kisiasa.

MAUDHUI  YATAKAYO  PEWA  KIPAUMBELE

Maudhui  yatakayo pewa  kipaumbele  katika  program  hii  ni  pamoja :
1.    Riwaya  mbalimbali  za  kusisimua
2.     Simulizi  kuhusu  historia  ya  ukweli  ya maisha (  IWE SIMULIZI  YENYE  KUSISIMUA )
3.    Mafundisho  mbalimbali  ya  ujasiriamali kama  vile  :
i.                   Utengenezaji  na  utayarishaji wa  bidhaa  mbalimbali
ii.                 Ufugaji wa  mifugo   mbalimbali  kama vile  kuku  wa  kienyeji, kuku wa  nyama na kuku wa mayai, mbuzi  wa nyama & maziwa, ng’ombe  wa  nyama na maziwa, nakadhalika.
iii.             Kilimo  cha  mazao  mbalimbali ya  chakula  na  biashara
iv.             Fursa  za  biashara  mbalimbali   na  ujasiriamali
v.                 Uanzishaji  na  uendeshaji  wa  biashara  mbalimbali
vi.              Uanzishaji  na  uendeshaji  wa  makampuni  mbalimbali
vii.          Uanzishaji  na  uendeshaji  wa  Taasisi  na  mashirika  mbalimbali
viii.       Uanzishaji  na  uendeshaji wa  viwanda  vidogo  vidogo  vya  aina  mbalimbali  kama  vile  viwanda  vya usindikajiwa  bidhaa  mbalimbali  nakadhalika.
ix.             Usagaji  na  upakiaji wa  unga  wa  mahindi, muhogo nakadhalika.
x.                Uanzishaji na uendeshaji  wa  biashara  ndogo  za  aina  mbalimbali .
xi.             Mafunzo  ya  ufundi  stadi.
4.    Uandishi  wa  vitabu  vya  kitaaluma  vya  masomo mbalimbali  kuanzia  ngazi  ya  chekechea.
5.    Uandishi  kuhusu  umuhimu  na faida  za  kusoma  kozi  mbalimbali  kuanzia  ngazi  ya  cheti  nakuendelea  zinazo  tolewa  na  vyuo  mbalimbali
6.    Uandishi  kuhusu historia  na shughuli  za   Taasisi  mbalimbali  zisizo  kuwa  za  kiserikali (NGOS)
7.    Uandishi  kuhusu   historia  na shughuli  za  kampuni  mbalimbali 
8.    Uandishi  kuhusu  utelekezaji  wa  miradi  ya  mashirika  mbalimbali  yasiyokuwa  ya  kiserikali ( NGOS )
9.    Vitabu   kuhusu   mafundisho  ya  kidini
10.                       Vitabu  kuhusu    mafundisho  ya  afya
11.                       Vitabu  kuhusu  masuala  ya  jadi  na  utamaduni
12.                       Uandishi  wa  mashairi ya  muziki wa  bongo fleva ( Katika  maudhui  mbalimbali  kuanzia   R& B  hadi  HipHop ) :HII  INAWAHUSU  WATUNZI WA  MASHAIRI YA  NYIMBO ZA  BONGO  FLEVA  AMBAO  WANATAKA  KUONYESHA  VIPAJI  VYAO  VYA  UTUNZI KUPITIA  KITABU  )
13.                       NAKADHALIKA.

JINSI   YA   KUFANYA
Fika  katika  ofisi zetu  zilizopo  MBEZI  BEACH  jijini  DAR ES  SALAAM  ukiwa na manuscript ( muswaada)  wa kitabu  chako  katika  soft copy .
NA   KWA  MAELEZO NA  UFAFANUZI ZAIDI, WASILIANA  NASI  KWA  SIMU  NAMBA : 0687319762
Kwa  waandishi chipukizi  waliopo  nje  ya mkoa  wa  Dar Es  Salaam, ambao  wanataka  kushiriki  katika  program  hii  wasiliana  nasi kwa simu  yetu  0687319762  tuwape utaratibu.
WAHI  NAFASI  YAKO  MAPEMA,KABLA   OFA  HII  HAIJA FIKA  TAMATI.


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni